Tuesday, 3 March 2015

VIONGOZI WA CCM TAIFA WAWASILI MJINI SONGEA TAYARI KWA MAZISHI YA MAREHEMU CAPTAIN KOMBA


Katibu mkuu wa CCM Taifa Mh. Abdulhaman Kinana akiwasili Mjini Songea leo kwa ajili mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Mbinga Mgharibi Mh. John Komba




Naibu katibu mkuu wa CCM Taifa na naibu waziri wa Fedha wa Tanzania Mh. Mwigulu Nchemba wakisalimiana na wakazi wa mjini Songea alipowasili kwa ajili ya mazishi ya marehemu John Komba. 

Mwanamuziki mashuhuru wa Taarabu Bi. Khadija Kopa akiwasili mjini Songea leo



MKUU WA MKOA WA RUVUMA AKIWAONGOZA WANANCHI WA SONGEA KUAGA MWILI WA MAREHEM JOHN KOMBA

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma akiongoza maelfu ya wakazi wa Songea kutoa salam za rambi rambi za mkoa

MWILI WA MH. CAPTAIN JOHN KOMBA WAWASILI MJINI SONGEA


Mwili wa marehemu John Komba ambae alikuwa Mbunge wa Mbinga Magharibi na mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM ukiwasili kwenye uwanja wa ndege mjini Songea leo.

KATIBU MWENEZI WA CCM TAIFA MH. NAPE MNAUYE AKISHIRIKI KATIKA WIMBO WA KUMUAGA MAREHEMU CAPTAIN KOMBA




Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Mh. Nape Nnauye, Mbunge wa Viti Maalum na mkoa wa Singida Martha Mlata wakishirikiana na mwanamuziki mkongwe King Kikii, Lwiza Mbutu na wasanii wengine kuimba wimbo maalum wa kumuenzi marehemu Kapteni John Komba wakati wa kutoa heshima za mwisho kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.

Tarehe 2 Machi 2015.

NAPE AONGOZA WANAMUZIKI WA DANSI KUIMBA WIMBO MAALUM WA KUMUENZI KAPTENI...

Friday, 7 November 2014

DANGOTE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KIWANDA CHAKE KIKUBWA CHA SARUJI MJINI MTWARA

Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote (kulia) mfanyabiashara maarufu kutoka Nigeria, akiteremka toka kwenye ndege alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara, kwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda kikubwa cha saruji kinachojengwa mkoani humo.

Dangote akilakiwa na Mwakilishi Mkazi wa kampuni hiyo nchini, Esther Baruti (kushoto)

Dangote akisalimiana na Balozi Mdogo wa Nigeria nchini, Adamu Mussa

Dangote akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa kampuni ya Dangote nchini, Esther Baruti na Balozi Mdogo wa Nigeria nchini, Adamu Mussa.

Dangote akisalimiana na wafanyakazi wa kampuni inayojenga kiwanda hicho ya Dil & Sinoma, baada ya kuwasili eneo la ujenzi wa kiwanda.

Alhaji Aliko Dangote akitabasamu baada ya kuwasili eneo la ujenzi wa kiwanda hicho.
Dangote akitumia gari kukagua ujenzi wa kiwanda hichoMwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote akiwa kwenye gari huku akipata maelezo ya ujenzi wa kiwanda hicho kutoka kwa mafundi na wahandisi ya Dil & Sinoma inayojenga kiwanda hicho kitakachokuwa cha tatu kwa ukubwa Afrika.

Msafara wa Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote, ukikagua ujenzi wa kiwanda hicho kinachotarajiwakuanza kazi Aprili, mwakani. Awamu ya kwanza ya kiwanda hicho ujenzi wake ukikamilika kitakuwa kinazalisha tani 6000 kwa siku.

Dongote akiagana na Kaimu Mkuu wa Mkoawa Mtwara, Ponsiano Nyami

Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote, akiaga alipokuwa akiondoka na ndege yake kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara jana. Alitumia takribani saa mbili kuwepo nchini, baada ya kuwasili asubuhi saa 1:42 na kuondoka saa 3:42 baada ya kupata maelezo ya ujenzi na kukagua kiwanda chake.

Thursday, 6 November 2014

MH. RAIS KIKWETE WAAPISHA MAKATIBU WAKUU, MABALOZI, WAKUU WA MIKOA PAMOJA NA MAKATIBU TAWALA WAPYA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mh. Samwel William Shellukindo kuwa Balozi na Msaidizi wa Rais katika Masuala ya Diplomasia leo Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mh. John Vianney Mongella kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera leo Ikulu jijini Dar es salaam.

Mkuu waRais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mh. Halima Omary Denengo kuwa Mkoa wa Mtwara leo Ikulu jijini Dar es salaam.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Dkt Ibrahim Hamisi Msangi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi leo Ikulu jijini Dar es salaam.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpatia vitendea kazi Dkt Yohana Budeba kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpa vitendea kazi Injinia Mbogo Futakamba kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpa vitendea kazi Dkt Donan Mmbando kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpa vitendea kazi Mhe Jack Mugendi Zoka kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpa vitendea kazi Mhe Charles Pallangyo kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Geita Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akumuapisha na kumpa vitendea kazi Bw, Adoh Stephen Mapunda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 6, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wapya baada ya kuwaapisha Ikulu jijini Dar es salaam leo.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Balozi mpya wa Tanzania Nchini Canada Mhe. Jack Mugendi Zoka (wa pili kushoto), pamoja na mabalozi wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambao ni kutoka kushoto Balozi Joseph Sokoine (Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika). Balozi Yahaya Simba (Mkurugenzi idara ya Mashariki ya Kati na Balozi Celestine Mushi, Mkurugenzi wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa.

HAKATI ZA KUMPATA KIONGOZI WA KIRAIA WA MPITO ZAANZA NCHINI BURKINA FASO

Mkutano wa wadau katika mchakato wa kutafuta serikali ya mpito ya Burkina Faso

Wanadiplomasia wanaowawekea shinikizo viongozi wa jeshi la Burkina Faso kukabidhi madaraka kwa raia, wameanza mchakato wa kumtafuta mtu atakayeongoza serikali ya mpito hadi uchaguzi utakapofanyika.
MMazungumzo hayo ya jana yalisimamiwa na Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria, John Dramani Mahama wa Ghana na Macky Sall wa Senegal, yakiwashirikisha maafisa wa jeshi, viongozi wa vyama vya kisiasa na wawakilishi wa asasi za kiraia.

Ingawa washiriki waliafikiana juu ya kuwepo kwa utawala wa mpito kwa kipindi cha mwaka mmoja, ambao utaongozwa na raia, hakukuwapo makubaliano juu ya kiongozi wa kipindi hicho. Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliwaachia jukumu hilo wahusika nchini Burkina Faso.
''Na mtaendelea hadi pale mtakapompata mtu kutoka nchi hii, mwenye haiba, heshima, uaminifu na uzalendo ambaye ataweza kuiongoza Burkina Faso hadi mwakani, kwenye uchaguzi huru, wa haki na wa kuaminika. Hilo ndilo jukumu tunalowaachia kutekeleza.'' Alisema rais Mahama.

Rai ya kuepuka vikwazo


Rais wa Ghana John Dramani Mahama akitoa rai katika mkutano huo

Rais Mahama alisema anaamini mchakato wa kumpata kiongozi huyo hautachukuwa wiki kadhaa, na kueleza matumaini yake kwamba haitakuwa lazima kwa jumuiya ya kimataifa kuiwekea vikwazo Burkina Faso. Umoja wa Afrika uliwapa wanajeshi wa Burkina Faso muda wa wiki mbili kukabidhi madaraka kwa raia, la sivyo wakabiliwe na vikwazo vya kiuchumi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon aliunga mkono juhudi za marais hao kutafuta suluhisho la amani katika mzozo huo wa Burkina Faso. Msemaji wake Stephen Dujarric amesema Umoja wa Mataifa unashirikiana na Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, kutafuta suluhisho la kudumu linalowahusisha wadau wote nchini humo.

Hali kadhalika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema pia linaunga mkono mchakato huo, na kuwataka wanajeshi kukabidhi madaraka na kuheshimu katiba ya nchi bila kuchelewa.

Ishara ya mvutano


Luteni Kanali Isaac Zida anayeshinikizwa kukabidhi madaraka kwa viongozi wa kiraia

Hata hivyo katika kile kilichochukuliwa kama ishara ya kupanda kwa joto la mvutano katika mkutano huo, wanasiasa wa upinzani pamoja na wanaharakati walitoka nje baada ya maafisa wa chama kilichokuwa madarakani kuingia katika mkutano huo.
Kiongozi wa asasi za kiraia Mathias Tankoano alisema hawawezi kukaa chumba kimoja na watu wanaotuhumiwa kusababisha vifo vya watu ambao hata bado hawajazikwa, na kuongeza kuwa maafisa hao wanapaswa kuhukumiwa kwa vifo hivyo, na kwa hila zao dhidi ya katiba ya nchi ambazo zililipeleka taifa katika ghasia.

Taarifa zilizotolewa baadaye zilisema Assimi Kouanda, kiongozi wa chama cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore alikamatwa na polisi baada ya kutoa matamshi ambayo yanaweza kuvuruga utulivu wa umma.
Burkina Faso iliingia katika mzozo wiki iliyopita baada ya kuibuka kwa maandamano yenye ghasia, kufuatia hatua ya aliyekuwa rais wake Blaise Compaore kujaribu kubadilisha katiba ili aweze kugombea mhula mwingine, kuendeleza utawala wake wa miaka 27. Baada ya kiongozi huyo kuikimbia nchi, aliyekuwa naibu kamanda wa kikosi cha kumlinda, Luteni Kanali Isaac Zida aliteuliwa na jeshi kuchukua madaraka ya kuiongoza nchi hiyo.

MH. KINANA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA NCHINI TANZANIA,


Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (kulia) akimkaribisha Balozi wa Rwanda hapa nchini bwana Eugene Kayihura, kabla ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa Balozi huyo Ernest Bugingo.


Balozi wa Rwanda hapa nchini Eugene Kayihura, akijitambulisha kwa Katibu Mkuu wa CCM Mh. Abdulrahman Kinana, kabla ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Balozi huyo Ernest Bugingo.


Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa katika mazungumzo na Balozi huyo.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (kushoto) akimsindikiza mgeni wake Balozi wa Rwanda hapa nchini Eugene Kayihura, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Balozi huyo Ernest Bugingo.

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (kulia) akiagana na Balozi wa Rwanda hapa nchini Eugene Kayihura, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.

Wednesday, 5 November 2014

SEMINA YA SDG'S IKIENDELEA



Mhadhiri wa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Osward Mashindano akifafanua umuhimu wa kuwashirikisha wananchi wa ngazi ya chini kuhusu maswala ya malengo ya milenia ili yaweze kufikiwa kwa urahisi zaidi.