![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiBLT_vdrO9O2L9a7YAW0hi5ejtuQcFvttTlN4tyhw467KU8UnxrARJvJejPCdYYQccLf0lrnzGqOM9YEK_l_2geG6-_dza3wQvhE-t4DcXbEiE9TaqIOvZLjz_2hfDP3JdGG-S2YfASzO/s640/01.JPG)
Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote (kulia) mfanyabiashara maarufu kutoka Nigeria, akiteremka toka kwenye ndege alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara, kwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda kikubwa cha saruji kinachojengwa mkoani humo.
Dangote akilakiwa na Mwakilishi Mkazi wa kampuni hiyo nchini, Esther Baruti (kushoto)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgp-nQox0XLoTnwdJOG6dbcX7gndlAkS_cgBLPERbvGAj4SkrfqiDKnxJJeW6GCLEZkRV0nzHbGLH9n0CjBIuuJtSWIs5C_mWavBA7FO2ax6O9UohmAx5kWDy3YhZsgULePavI15mUIqAqx/s640/IMG_0907.JPG)
Dangote akisalimiana na Balozi Mdogo wa Nigeria nchini, Adamu Mussa
Dangote akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa kampuni ya Dangote nchini, Esther Baruti na Balozi Mdogo wa Nigeria nchini, Adamu Mussa.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiODckjJCYxpaRxVuKLaZCQ-8r8FX8V1iIBPslH5c3pka0TPB9KMYXz4TdWtNWl_-AjdC-VNeCMqiBqPxJE_VBe9bQKAv5AvGpUGqTmWuaOIetFmM8RAaiV9FTVSoJdm7BV4zzGijXHCUjh/s640/IMG_0970.JPG)
Dangote akisalimiana na wafanyakazi wa kampuni inayojenga kiwanda hicho ya Dil & Sinoma, baada ya kuwasili eneo la ujenzi wa kiwanda.
Alhaji Aliko Dangote akitabasamu baada ya kuwasili eneo la ujenzi wa kiwanda hicho.
Dangote akitumia gari kukagua ujenzi wa kiwanda hicho
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh-CDn1FXH_7BQj9N9cEkL9BwoBXaWFbLrBNjSHog-R2Hm7xYBfuL34oP-R6c6pZntTW8NUr0UqerxWu0KSM3URwoEs-0uWk8xrMiVilMyQK4vt2THeGsMppr-iT08uRGNQ0iw9RafNJPzP/s640/IMG_1017.JPG)
Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote akiwa kwenye gari huku akipata maelezo ya ujenzi wa kiwanda hicho kutoka kwa mafundi na wahandisi ya Dil & Sinoma inayojenga kiwanda hicho kitakachokuwa cha tatu kwa ukubwa Afrika.
Msafara wa Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote, ukikagua ujenzi wa kiwanda hicho kinachotarajiwakuanza kazi Aprili, mwakani. Awamu ya kwanza ya kiwanda hicho ujenzi wake ukikamilika kitakuwa kinazalisha tani 6000 kwa siku.
Dongote akiagana na Kaimu Mkuu wa Mkoawa Mtwara, Ponsiano Nyami
Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Group of Industries), Alhaji Aliko Dangote, akiaga alipokuwa akiondoka na ndege yake kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara jana. Alitumia takribani saa mbili kuwepo nchini, baada ya kuwasili asubuhi saa 1:42 na kuondoka saa 3:42 baada ya kupata maelezo ya ujenzi na kukagua kiwanda chake.